WATU 2 WAFARIKI DUNIA NA WENGINE 18 WANUSURIKA KUFUNIKWA NA KIFUSI- GEITA. - KABONGE BLOG.

Blog hii ni kwaajili ya masuala/taarifa za kidini na matukio yanayotokea kila siku.

Breaking

Sunday, October 23, 2016

WATU 2 WAFARIKI DUNIA NA WENGINE 18 WANUSURIKA KUFUNIKWA NA KIFUSI- GEITA.

WATU wawili wamefariki Dunia na 18 kunusurika na wakijeruhiwa vibaya sehemu mbalimba ya miili yao baada ya kufukiwa na kifusi wakati wakichimba mawe yanadhaniwa kuwa na dhahabu.

Tukio hilo la kusikisitisha na liloacha simanzi kwa wananchi limetokea usiku wa kuamkia jumatano majira ya saa tano usiku katika kitongoji cha Ishimba kijiji na kata na Nyamalimbe wilaya  na mkoa  wa Geita.

Wakizungumza na Channel Ten iliofika kijijini hapo na kushudia tukio hilo baadhi ya wachimbaji wamesema kuwa waliofaliki ni Paul Musa (3o) mkazi wa Msoma  Costantine  Samweli( 37) mkazi wa Chato na wote walikuwa ndani ya shimo hilo.

Pamoja na kutokea tukio la wachimbaji hao kupoteza maisha na wengine kujiruhiwa baadhi ya wachimbaji  wameomba serikali ya awamu ya tano kuwapatia maeneo ya kuchimba na kuwapa dhana za kisasa.

Mwenyekiti wa kijiji hicho Jonadhani Muogota amesema kuwa watu waliokuwa kwenye shimo hilo walikuwa ni wengi lakini wengi wao walitoka mapema na jitiada za kuwaokoa  wawili ziaendelea.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Geita mponjli Mwabulambo alipotafutwa kuzungumzia tukio hilo kwa njia ya simu alikuwa haya.

Pamoja na eneo hilo kudaiwa kumilikiwa na kampuni ya Mwamba Resources ltd kwa ajili ya utafiti lakini inadaiwa kuwa kampuni hiyo inachukua asilimia 60 kutoka kwa wachimbaji wadogo huku kijiji kikichukua asilimia 40.

No comments:

Post a Comment