KAMANDA SIRRO ASHIKA SILAHA ZOTE ZA WAHARIFU KIBITI. - KABONGE BLOG.

Blog hii ni kwaajili ya masuala/taarifa za kidini na matukio yanayotokea kila siku.

Breaking

Sunday, December 3, 2017

KAMANDA SIRRO ASHIKA SILAHA ZOTE ZA WAHARIFU KIBITI.

MKUU wa jeshi la polisi nchini (IGP)Simon Sirro amewahakikishia wananchi mkoani Pwani kuwa silaha zote zilizochukuliwa na wahalifu wa ovyo ovyo huko Kibiti na Mkuranga zimerudi zote mkononi mwa dola na kusambaratisha mtandao wa kiuhalifu .

Aidha ametoa rai kwa wazazi na walimu kutoa taarifa kwenye vituo vya polisi mara watakapobaini kuna mwanafunzi mtoro ama hajaripoti shule kwa miezi kadhaa kwani wapo baadhi ya watoto wanaotumika kufundishwa uhalifu hata wakutumia silaha na watu wasiowema.

Pamoja na hayo IGP Sirro ,amesema vyombo vya ulinzi na usalama nchini vinashirikiana na nchi ya Msumbiji kupambana na wahalifu waliobainika kukimbilia nchini  humo wakitokea Tanzania.

Aliyasema hayo wilayani Kibaha ,mkoani Pwani ,katika ziara yake ya kikazi ya siku moja ambapo pia alizungumza na viongozi wa mashirika ya umma,wazee maarufu ,wastaafu mbalimbali na kamati ya ulinzi na usalama mkoani hapo.

IGP Sirro alieleza kuwa ,vyombo vya ulinzi na usalama vinaendelea kupambana na yeyote atakaekuja kwa moto nae wataenda nae kwa moto na atakaekuja baridi wataenda nae baridi.

Alisema serikali imeshinda kwa hilo na hali kwa sasa ni shwari katika wilaya hizo.

IGP Sirro alieleza amepatiwa taarifa ya wanafunzi zaidi ya 1,300 mkoani hapo kuwa ni watoro na hawajulikani walipo hivyo wazazi washirikiane kusaidia jeshi la polisi kujua walipo.

No comments:

Post a Comment