HISTORIA FUPI YA IBADA YA ROZALI TAKATIFU. - KABONGE BLOG.

Blog hii ni kwaajili ya masuala/taarifa za kidini na matukio yanayotokea kila siku.

Breaking

Sunday, October 1, 2017

HISTORIA FUPI YA IBADA YA ROZALI TAKATIFU.

Utangulizi
Katika Kalenda ya Kanisa Katoliki, huwa mwezi wa tano na mwezi wa kumi ni miezi ambayo imewekwa kwa ajili ya Bikira Maria na Mama Kanisa. Hivyo hiyo miezi huwa inasaliwa rozari. Wengi waweza kujiuliza kuwa ni kwa nini ifanyike miezi hiyo? Yafuatayo ni majibu, mwezi wa tano umewekwa kwa heshima ya Bikira Maria kutokana na nini kilitokea katika historia hapo nyuma. Mnamo Karne ya 16 mwezi watano kwa miaka yote ulikuwa ni mwezi ambao sikukuu nyingi za kiserikali ndo zilikuwa zikifanyika. Kanisa kwa kutambua hilo nalo likahidhinisha pia mwezi wa tano uwe ni mwezi wa Rozari, na kwa makusudi zaidi Kanisa lililenga kuwa sherehe hizo ziendane na taratibu za wakristu, ni kwa msingi huo sherehe hizo ziliendana na mwezi wa rozari na kutokea hapo ikahidhinishwa kuwa mwezi wa tano wa mwaka ni mwezi wa Bikira Maria. Pia mwezi wa kumi (October) pia ni mwezi wa Bikira Maria na pia ni mwezi wa Kusali Rozari kutokana na historia ya hapo nyuma pia, na ilikuwa kwamba baada ya ushindi wakristo walioupata katika vita baina yao na yule aliyeitwa Lepanto mnamo 7 October, 1571, Papa wa wakati ule Papa Pius V aliufanya huo ushindi kuwa ulitokana na maombezi ya Bikira Maria, na alisema kuwa rozari ni silaha kubwa hata kuliko silaha kubwa za kivita. Ni Kwa msingi huu tunaona kuanzia hapo mwezi wa kumi ukawa mwezi uliotengwa na Mama Kanisa kwa Bikira Maria, na pia ukaitwa mwezi wa Rozari.
Historia yenyewe
Ni kwamba sala ya Rozari inasemekana kuanzishwa na Mt. Dominico aliyezaliwa mnamo mwaka 1170 na kufariki mwaka 1221 na hiyo sala Mt. Dominico aliipata kwa njia ya ufunuo ambapo Bikira Maria alimtokea na kumwamuru awe anasali rozari. Bikira Maria alimwamuru mtakatifu Dominico kusali rozari kwa kipindi hicho iwe kama silaha yake ili kupambana na uzushi uliokuwa umeibuka ukipingana na mafundisho ya Kanisa, na huo uzushi uliitwa ‘ Albigensia’ hili ni kundi lilokuwa na imani kuwa Duniani kuna nguvu nguvu mbili zenye uwiano sawa lakini hupingana na kupigana moja baada ya nyingine, nazo nguvu hizo ni Mungu na Shetani. Hivyo hawa waliamini kabisa kuwa Mungu na Shetani wana nguvu sawa ( Dualistic ) waliamini pia kuwa dunia hii imejaa uovu kwa kuwa iliumbwa na mwovu. Ni kwa msingi huu Kanisa liliamua kupambana na hawa wazushi ambao pia walionekana kupotosha mafundisho ya Kanisa. Ndipo tunaona Bikira Maria anamtokea Mtakatifu Dominico na kumwambia asali rozari ili kupambana na mafundisho hayo ya kizushi. Ni Papa Pio V ambaye mnamo mwaka 1569 alihidhinisha rasmi kusali rozari kwa kanisa nzima na kuhidhinisha rozari iwe jinsi tunavyoiona sasa. Katika zile zama za kati, watawa wamonaki walizoea kusali zaburi 150, na kwa upande wa waumini walei ambao kwa kipindi hicho hawakujua kusoma zaburi iliwabidi wasali sala ya Baba yetu mara 150 baadala ya zaburi 150 na hizo baba yetu walizisali kwa kuhesabu punje 150 zilizokuwa zimefungwa kwenye kamba ndefu ambayo kwa lugha ya kitaalamu iliitwa “ Corona” au kwa Kiingereza “ Crown” kadiri ibada kwa Bikira Maria ilivyoendelea kushamiri mnamo Karne ya 12, sala kwa Bikira Maria ilianzishwa na hivyo kuanza kusali salamu maria 150 baadala ya baba yetu 150.
Salamu Maria 150 hapo baadaye zilikuja kugawanywa katika makundi/ mafungu na Mtawa mdominica aliyeitwa Henry Kalkar ( 1328-1408), ambapo kila tendo la rozari lilikuwa na mafungu 50 ya salamu Maria ambapo pia kila fungu liligusia maisha ya Bikira Maria na Yesu katika historia ya wokovu wetu. Zaidi ya hapo, mtawa mwingine wa mdominican aliyeitwa Alanus de Rupe aliendelea kugawanya hiyo historia ya matendo ya wokovu wetu katika matendo ya furaha,uchungu, na utukufukama tunavyoyaona sasa. (NB Matendo ya mwanga hayo ni ya majuzi siyo ya wakati ule). Na nikuanzia hapo Bikira Maria amepewa nafasi kubwa katika shirika la watawa wa Dominican. Hivyo utamaduni wa kusali rozari umeendelea karne hata karne, mfano Papa Leo XIII (1878-1903) aliweka msisitizo mkubwa juu ya ibada ya rozari kwa Bikira Maria. Kuanzia September 1, 1883 Baba Mtakatifu Leo XIII aliandika jumla ya barua za kichungaji 11 zote zikiwa zinaweka mkazo juu ya rozari. Hivyo rozari ni sala inayotokana na maandiko matakatifu( Biblia). Mafumbo ya rozari yote yanapatikana katika agano jipya ambapo ndo tunaona matendo ya Bikira Maria na Yesu Kristo katika wokovu wetu.
tunakumbushwa uchungu aliopata Bikira Maria Katika maisha yake hasa ule utabiri wa Simeoni kwa Bikira Maria juu ya mateso na kifo cha mwanae Yesu, Matendo saba ya furaha kwa Maria ambapo yaananza na kupashwa habari kwa Bikira Maria na Malaika wa Bwana, kupalizwa mbinguni, na matendo ya huruma ya Bikira Maria kwa wale ambao wanaendelea kuteseka hapa duniani.



*_ROZARI TAKATIFU_*


          🔵🔵 🔵
       ðŸ”µ             🔵
      🔵              ðŸ”µ
      🔵            ðŸ”µ
      ⚫ *_T.4_*   🔵
      🔵         ⚫ *_T.3_*
      🔵            ðŸ”µ
    🔵                ðŸ”µ
  🔵                   🔵
 ðŸ”µ                    ðŸ”µ
 ðŸ”µ                   🔵
 ðŸ”µ                 🔵
 ðŸ”µ                ðŸ”µ
 ðŸ”µ               🔵
🔵               🔵
⚫ *_T.5_*     🔵
 ðŸ”µ          ⚫ *_Tendo 2_*
  🔵         🔵
   ðŸ”µ          ðŸ”µ
    🔵          ðŸ”µ
    🔵         🔵
    🔵        ðŸ”µ
  🔵         🔵
  🔵         🔵
   ðŸ”µ       🔵
    🔵    ðŸ”µ
      💮🔵
   ⚫ *_Tendo 1_*
   ðŸ”µ
     ðŸ”µ
       ðŸ”µ
        ⚫ *_Baba yetu_*
         ðŸ”º
          ◻
    ◻✝◻ *_Nasadiki_*
          ◻
          ◻


*MAELEZO*

🔵 _Salamu Maria_
⚫ _Mafumbo ya Rozari_

*_N.b_*
*```Kabla ya kutaja tendo, utasali atukuzwe Baba kisha sala ifuatayo```*


_Ee Yesu Mwema, utusamehe dhambi zetu, utukinge na moto wa milele,, ongoza roho zote mbinguni, hasa za wale wanaohitaji zaidi huruma yako,,,,,, Tunaomba hayo yote kwa njia ya Yesu Kristo bwana wetu_


*SALA MUHIMU*


*_Nasadiki / Apostles' Creed_*


*Nasadiki kwa Mungu baba Mwenyezi Muumba wa Mbingu na nchi na Kwa Yesu Kristo mwanaye wa pekee bwana wetu. Aliyezaliwa na* *Bikira Maria, kwa uwezo wa Roho mtakatifu. Akateswa kwa mamlaka ya Ponsio Pilato, Akasulubiwa, akafa,*
*akazikwa na kushukia kuzimu. Siku ya tatu* *akafufuka katika wafu, akapaa mbinguni, Amekaa kuume kwa baba na atakuja tena kwa utukufu*
*kuwahukumu wazima na wafu.*
*Nasadiki kwa roho mtakatifu, Kanisa takatifu Katoliki ushirika wa* *watakatifu,maondoleo ya dhambi, ufufuko wa miili na uzima wa milele AMINA.*


*_Baba Yetu / Our Father / Pater Noster_*

*Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe. Ufalme wako ufike.*
*Utakalo lifanyike duniani kama mbinguni.*
*Utupe leo mkate wetu wa kila siku.*
*Utusamehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea.*
*Usitutie katika kishawishi, lakini utuopoe maovuni. Amina.*


*_Salamu Maria / Hail Mary / Ave Maria_*


*Salamu, Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe, umebarikiwa kuliko* *wanawake wote, na Yesu, mzao wa tumbo lako amebarikiwa.*
*Maria mtakatifu, Mama wa Mungu,*
*Utuombee sisi wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.*


*_Atukuzwe Baba / Glory Be_*


*Atukuzwe Baba, na Mwana na Roho Mtakatifu.*
*Kama mwanzo, na sasa, na siku zote, na milele. Amina.*



*MATENDO YA FURAHA*

 ( _Jumatatu na Jumamosi_ )

1. *Tendo la kwanza;* _Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu._


2. *Tendo la pili;* _Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti. Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani._


3. *Tendo la tatu;* _Yesu anazaliwa Betlehemu. Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara_



4. *Tendo la nne;* _Yesu anatolewa hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo._


5. *Tendo la tano;* _Maria anamkuta Yesu hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu._



*MATENDO YA UCHUNGU*

 ( _Jumanne na Ijumaa_)


1. *Tendo la kwanza;* _Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi._


2. *Tendo la pili;* _Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu._


3. *Tendo la tatu;* _Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi._


4. *Tendo la nne;* _Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu._


5. *Tendo la tano;* _Yesu anakufa Msalabani. Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria._



*MATENDO YA UTUKUFU*

 ( _Jumatano na Jumapili_)


1. *Tendo la kwanza;* _Yesu anafufuka. Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu._


2. *Tendo la pili;* _Yesu anapaa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni._


3. *Tendo la tatu;* _Roho Mtakatifu anawashukia Mitume. Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu._



4. *Tendo la nne;* _Bikira Maria anapalizwa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri._


5. *Tendo la tano;* _Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema._



*MATENDO YA MWANGA* 

         ( _Alhamisi_)


1. *Tendo la kwanza;* _Yesu anabatizwa Mto Jordani. Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo._


2. *Tendo la pili;* _Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana. Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya injili._


3. *Tendo la tatu;* _Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli._


4. *Tendo la nne;* _Yesu anageuka sura. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuung’arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu._


5. *Tendo la tano;* _Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristi. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine._


*SALAM, MALKIA!*

*_Salam, Malkia! Mama mwenye huruma uzimatulizo matumaini yetu._* *_Salam!_* *_Tunakusihi ugenini sisi wana wa Eva. Tunakulilia tukilalamika na kuhuzunika huku bondeni kwenye machozi._* *_Haya basi mwombezi wetu utuangalie kwa macho yako yenye huruma,_* *_Na mwisho wa ugeni huu utuonyeshe Yesu mzao mbarikiwa wa tumbo lako. Ee mpole, Ee mwema, Ee mpendelevu Bikira Maria._*

*K. Utuombee mzazi mtakatifu wa Mungu!*
*_W. Tujaliwe ahadi za Kristo_*

*LITANIA YA BIKIRA MARIA*

_Bwana utuhurumie. *Bwana utuhurumie.*_

_Kristo utuhurumie.
*Kristo utuhurumie.*_

_Bwana utuhurumie. *Bwana utuhurumie.*_

_Kristo utusikie. *Kristo utusikilize.*_

_Baba wa mbinguni, Mungu, *utuhurumie.*_

_Mwana Mkombozi wa dunia, Mungu, *utuhurumie.*_

_Roho Mtakatifu, Mungu, *utuhurumie.*_

_Utatu Mtakatifu, Mungu mmoja, *utuhurumie*._

_Kiitikio:_ *Utuombee*

_Maria Mtakatifu,_
_Mzazi Mtakatifu wa Mungu,_ 
_Bikira Mtakatifu, Mkuu wa mabikira,_
_Mama wa Kristu,_
_Mama wa neema ya Mungu,_
_Mama mtakatifu sana,_
_Mama mwenye usafi wa moyo,_
_Mama usiye na doa,_
_Mama usiye na dhambi,_
_Mama mpendelevu,_
_Mama mstaajabivu,_
_Mama wa shauri jema,_
_Mama wa Mwumba,_
_Mama wa Mkombozi,_
_Bikira mwenye utaratibu,_
_Bikira mwenye heshima,_
_Bikira mwenye sifa,_
_Bikira mwenye enzi,_
_Bikira mwenye huruma,_
_Bikira amini,_
_Kikao cha haki,_
_Kikao cha hekima,_
_Sababu ya furaha yetu,_
_Chombo cha neema,_
_Chombo cha heshima,_
_Chombo bora cha ibada,_
_Waridi lenye fumbo,_
_Mnara wa Daudi,_
_Mnara wa pembe,_
_Nyumba ya dhahabu,_
_Sanduku la Agano,_
_Mlango wa mbingu,_
_Nyota ya asubuhi,_
_Afya ya wagonjwa,_
_Makimbilio ya wakosefu,_
_Mfariji wa wenye uchungu,_
_Msaada wa Wakristu,_
_Malkia wa Malaika,_
_Malkia wa Mababu,_
_Malkia wa Manabii,_
_Malkia wa Mitume,_
_Malkia wa Mashaidi,_
_Malkia wa Waungama,_
_Malkia wa Mabikira,_
_Malkia wa Watakatifu wote,_
_Malkia uliyeumbwa, pasipo dhambi ya asili,_
_Malkia uliyepalizwa mbinguni,_
_Malkia wa Rozari takatifu,_
_Malkia wa amani._
****

_Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia, *utusamehe, Bwana.*_


_Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia, *utusikilize, Bwana.*_


_Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia, *utuhurumie.*_

```K. Utuombee, Mzazi Mtakatifu wa Mungu.
W. Tujaliwe ahadi za Kristu.
```

_TUOMBE:_ *_Ee Bwana Mungu, utujalie sisi watumishi wako afya ya roho na ya mwili sikuzote. Tuopolewe na mashaka ya sasa kwa maombezi ya Maria mtakatifu, Bikira daima, ili tupate na furaha ya milele. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. Amina._*


*TUNAKIMBILIA ULINZI WAKO*


*Tunakimbilia ulinzi wako Mzazi Mtakatifu wa Mungu,  usitunyime tukiomba, tukiomba katika shida zetu;*
*utuokoe siku zote kila tuingiapo hatarini, ewe Bikira Mtukufu, Bikira Mtukufu mwenye baraka:*
*Amina*


No comments:

Post a Comment