MASOMO YA DOM YA 4 YA MWAKA 'A' WA KANISA. - KABONGE BLOG.

Blog hii ni kwaajili ya masuala/taarifa za kidini na matukio yanayotokea kila siku.

Breaking

Saturday, January 28, 2017

MASOMO YA DOM YA 4 YA MWAKA 'A' WA KANISA.

MASOMO YA MISA, JANUARI 29, 2017
DOMINIKA YA 4 YA MWAKA A

MWANZO:
Zab. 106:47

Ee Bwana Mungu wetu, utuokoe, utukusanye kwa kututoa katika mataifa, tulishukuru jina lako takatifu, tuzifanyie shangwe sifa zako.

SOMO 1
Sef. 2:3, 3:12 – 13

Mtafuteni Bwana, enyi nyote mlio wanyenyekevu wa dunia, ninyi mliozitenda hukumu zake; itafuteni haki, utafuteni unyenyekevu; huenda mtafichwa katika siku ya hasira ya Bwana.
Lakini nitasaza ndani yako watu walioonewa na masikini, nao watalitumainia jina la Bwana. Mabaki ya Israeli hawatatenda uovu, wala kusema uongo; wala ulimi wa hadaa hautaonekana kinywani mwao; kwa maana watakula na kulala, wala hapana mtu atakayewaogofya.

Neno la Mungu… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 146:6b – 10 (K) Mt. 5:3

(K) Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.

Huishika kweli milele.
Huwafanyia hukumu walioonewa,
Huwapa wenye njaa chakula;
Bwana hufungua waliofungwa. (K)

Bwana huwafumbua macho waliopofuka;
Bwana huwainua walioinama;
Bwana huwapenda wenye haki;
Bwana huwahifadhi wageni. (K)

Huwategemeza yatima na mjane;
Bali njia ya wasio haki huipotosha.
Bwana atamiliki milele,
Mungu wako, Ee Sayuni, kizazi hata kizazi. (K)

SOMO 2
1Kor. 1:26 – 31

Ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa; bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu; tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko; mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu. Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu hekima itokayo kwa Mungu, na haki, na utakatifu, na ukombozi; kusudi, kama ilivyoandikwa, Yeye aonaye fahari na aone fahari juu ya Bwana.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

SHANGILIO
Yn. 14:5

Aleluya, aleluya,
Tomaso akamwambia Bwana, Sisi hatujui uendako, nasi twaijuaje njia?
Aleluya.

INJILI
Mt. 5:1 – 12a

Yesu alipowaona makutano, alipanda mlimani; na alipokwisha kuketi, wanafunzi wake walimjia; akafumbua kinywa chake, akawafundisha, akisema,
Heri walio maskini war oho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.
Heri wenye huzuni; maana hao watafarijika.
Heri wenye upole; maana hao watairithi nchi.
Heri wenye njaa na kiu ya haki;
Maana hao watashibishwa.
Heri wenye rehema; maana hao watapata rehema.
Heri wenye moyo safi; maana hao watamwona Mungu.
Heri wapatanishi; maana hao wataitwa wana wa Mungu.
Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki; maana ufalme wa mbinguni ni wao.
Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu. Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristo.

No comments:

Post a Comment