MTANZANIA AIBUKA MSHINDI WA NNE KWENYE MASHINDANO YA UPISHI DUNIANI. - KABONGE BLOG.

Blog hii ni kwaajili ya masuala/taarifa za kidini na matukio yanayotokea kila siku.

Breaking

Friday, November 25, 2016

MTANZANIA AIBUKA MSHINDI WA NNE KWENYE MASHINDANO YA UPISHI DUNIANI.

Fred Uisso akiwa na Mratibu wa Taifa wa WORLD FOOD CHAMPIONSHIP Bi. Julie Haunn

 Mpishi mahiri wa Tanzania, Fred Uisso, ameibuka mshindi wa nne kwenye mashindano makubwa ya mapishi duniani (World Food Championship) yaliyofanyika huko Orange Beach, Alabama nchini Marekani, Nov 9 – 13.

Mshindi wa kwanza kwenye shindano hilo alipewa zawadi ya $300,000.

 Rais na CEO wa WFC, Mike Mc Cloud akimkabidhi tuzo Fred Uisso baada ya kuibuka mshindi wa nne

Kwenye picha hiyo juu aliyoweka Instagram, Uisso ameandika: Nikiwa na wafanyakazi wa Emirates airlines flight EK 212 from Texas to Dubai. Nilipata Heshima kubwa kwa rubani kuwatangazia abiria wote kuwa kwenye ndege hii Kuna WORLD CHEF CHAMPION NUMBER 4 na ilipigwa CHEERS👏👏👌 na abiria wote. Tnx again Emirates airlines for a kind hospitality. Kesho jumatatu saa 9 alasiri ntatua home na Emirates. MUNGU NI MWEMA SANA.”

No comments:

Post a Comment